APOSTLE GIDEON HEADER ANIMATIONS

SHOOTING MPYA YA WIMBO WA MTAKATIFU WA MTUME GIDEON MUTALEMWA

Ijumaa, 12 Julai 2013

APOSTLE GIDEON MUTALEMWA KUFANYA HUDUMA MAFINGA MKOA WA IRINGA

Mungu wetu ni Mungu ambaye hutumia watu wake kwa kazi yake. Katika waimbaji wote Mungu ameweza kumuona mtumishi wa Mungu Mtume Gideon Mutalemwa kwenda Iringa katika kanisa la Jerusalem Spiritual Transformation lililoko Lumwago Mafinga Iringa mjini siku ya tarehe 24 hadi 28/07/2013. Mtume Gideon Mutalemwa atakuwepo pale kwaajili ya kumwimbia Mungu na kumtangaza huyu Yesu tunayemtumikia kila siku.


Apostle Gideon Mutalemwa katika kanisa analoabudu la Yesu Kristo Huduma ya Maombezi na Uponyaji DSM

Mtume Gideon Mutalemwa ni muumini wa kanisa la Yesu Kristo la Huduma ya Maombezi na Uponyaji Mbezi Salasala kwa Nabii Flora hapa jijini Dar es Salaam. Ni Mtumishi mwenye mke mmoja ambaye ni mzawa wa Iringa na mtoto mmoja. Kwahiyo anapokuja huko Mafinga Iringa anakuja nyumbani.


Watu wa Iringa msipange wa kufikiria kukosa kufika Lumwago Mafinga maana Mungu wetu tunayemwamini ataenda kuonekana na kuhudumia miyo yote kwa kupitia karama aliyoweka kwa Mtume Gideon Mutalemwa.


Mungu amemuwezesha mtumishi kuwa na albamu yake inayoenda kwa jina la SAMBAMBA NA YESU na nadi ya albamu hii utweza kusikia na kuona nyimbo za kitamaduni na nyine nyingi zenye ujumbe mzuri wa Mungu.



Unaweza kuwasiliana na Gideo Mutalemwa kwa simu +255 719 697252 au kwa blogu hii www.apostlegideon.blogspot.com
KARIBUNI SANA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni